Visit Sponsor

Written by 2:41 pm KIMATAIFA Views: 4

RAIS TRAORE ANUNUA GRADERS ZAIDI YA 1000 NA MAGARI KUSAIDIA UJENZI WA BARABARA

BREAKING: Rais wa Burkina Faso Kapteni Ibrahim Traoré amenunua Graders zaidi ya 1,000 na magari mbalimbali ili kusaidia juhudi za ujenzi wa barabara kote Nchini Burkina Faso.

Jana, alikabidhi rasmi mitambo hiyo kwa timu zinazohusika na maendeleo na matengenezo ya miundombinu ya barabara nchini humo



Katika hotuba yake, Captain Traoré alisisitiza umuhimu wa kuwa na barabara bora kutoka mashambani hadi sokoni, akieleza kuwa barabara nzuri zitawawezesha wakulima kusafirisha mazao yao kwenda mijini kwa ufanisi zaidi na bila kuharibika.



Uwekezaji huu mkubwa katika maendeleo ya kitaifa unafanyika licha ya shutuma za awali kutoka kwa Jenerali Langley, ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Marekani Kamandi ya Afrika ambaye alidai kuwa Traoré anatumia vibaya akiba ya dhahabu ya nchi ya Burkina Faso kwa manufaa yake binafsi.

About The Author

(Visited 4 times, 4 visits today)

Last modified: April 25, 2025

Close