Visit Sponsor

Written by 4:11 pm BIASHARA Views: 16

NIC  INSURANCE  KWA KUSHIRIKIANA   NA EQUITY BENK KUTOA  MIKOPO YA KIDIGITAL.



Na Mwandishi  wetu Mwanahabari

Dar es Salam

Shirika la bima la taifa NIC INSURANCE yafanya makubaliano ya kufanya biashara na Benki ya Equity kutoa suluhisho la bima za kilimo na mikopo ya kidigitali.

Hayo yamesemwa  Jijini  Dar es laam  na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la bima la taifa NIC Insurance Bw. Kaimu Abdi Mkeyenge amesema  kuwa wamewekeza katika Benki ya Equity wananchi waweze kukopa ili kukuza na kuendesha shughuli za kiuchumi, lengo ni kuboresha sekta ya kilimo kwa kupata bima na mikopo rafiki.

“ushirikiano huu unaenda kusaidia kuleta faida na kutoa mchango kwa wananchi na kusaidia serikali kuwezesha mafanikio ya kiuchumi kwa wananchi mmojammoja.

Naye  Mkurugenzi Mtendaji wa Equity Benki Isabela Maganga amesema mteja anaweza kukopa na kupata bima ya maisha, biashara, nyumba na familia kwa ujumla ikiwa imetokea majanga mikopo unaweza kulipwa kupitia bima.


Tumetambua uwezo huo kupitia  shirika la bima la taifa  NIC na  kufanya  nao  kazi  bima la taifa ina uhitaji mkubwa wa masoko hususani kutoka kwa wafanyabiashara wa kilimo.

Aidha Wateja hao tunawafikia kidigatali zaid na tunatoa mikopo kutoka na kukua kwa mikopo yetu asilmia 75 pia mkopo huo unakuwa mtaji kwa mfanyabishara.

Vilevile tunaenda kuendelea kutoa bima kwa wafanyabaishara wote nchini na tunaenda kuhakikisha kutoa mikopo kwa wafanyabiashara wa kilimo na ajali za moto.

Tumeweka Mikakati hii na  malengo  mahususi ambayo tunaenda kuwafikia wafanyabiashara wengi kupata huduma zetu popote” amesema mkurugenzi maganga

About The Author

(Visited 16 times, 1 visits today)

Last modified: January 16, 2025

Close