Visit Sponsor

Written by 5:50 pm KITAIFA Views: 10

CHAMA CHA WANANCHI CUF YAWATAKA WAFANYABIASHARA KUTOPANDISHA BIDHAA SIKU YA MFUNGO WA RAMADHAN

Na Mwandishi Wetu MWANAHABARI

Chama cha wananchi-CUF kimetoa wito kwa wafanyabiashara wa bidhaa za chakula kutokupandisha bei ya bidhaa hizo ili wapate faida mara dufu wakati huu ambapo waumini wa dini ya kiislalm wakiwa katika mfungo wa Mwezi mtukukufu wa Ramadhan.



Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa chama hicho,Taifa Prof Ibrahim Lipumba alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar Es Salaam Leo jumapili March 2,2025 juu ya masuala mbalimbali.

Lipumba amesema kwa wakati huu ni vyema wafanyabiashara hao kuuza bidhaa za chakula kwa bei ambayo huwa wanauza ili waendeleze kupata thawabu kutoka kwa mwenyezi Mungu na si kuwakomoa wengine kwa kutaka faida kubwa.

Aidha Chama hicho pia kimewatakia waumini wote wa dini ya kiislam hapa nchini mfungo mwema wa mwezi mtukukufu wa Ramadhan

About The Author

(Visited 10 times, 3 visits today)

Last modified: March 2, 2025

Close