Visit Sponsor

Written by 12:39 pm KITAIFA Views: 100

POLISI 6 WASHIKILIWA KWA TUHUMA YA KUSABABISHA VIFO VYA WATU WAWILI

Kamanda Kanda Maalum Dar es salaam, SACP Jumanne Muliro akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani), Dar jana

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linawashikilia askari 6 wa jeshi hilo na walinzi 11 wa kampuni ya ulinzi ya Pasco Ltd  pamoja na maafisa misitu wawili  wakituhumiwa kusababisha vifo vya watu wawili maeneo ya Kiluvya, Dar es salaam Agosti 28, 2023.

Akizungumza na Wandishi wa Habari leo Agosti 29, 2023, Kamanda Kanda Maalum Dar es salaam, SACP Jumanne Muliro  amesema  tukio hilo lilitokea usiku wakati maafisa hao wakitimiza majukumu yao  ya kuhakikisha mazao ya misitu inalindwa na wanaofanya biashara hizo wanafuata taratibu ndipo wauza mkaa 30 wakakimbia na kuacha pikipiki zao.

“Baada ya muda kidogo walirudi na kuanza  kuwarushia mawe maofisa na makamanda wa polisi wakaanza purukushani.”alisema Muliro na kwamba miili ya marehemu  imehifadhiwa katika Hospitali ya Mloganzira na silaha zote zimechukuliwa kwa  ajili ya uchunguzi.

Watuhumiwa wote wanashikiliwa na jeshi la polisi na uchunguzi bado unaendelea.

About The Author

(Visited 100 times, 1 visits today)

Last modified: August 29, 2023

Close