Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohammed Mchengerwa, amemuelekeza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo kuhakikisha Muswada wa Sheria ya Usimamizi na Uendelezaji wa Makao Makuu Dodoma unawasilishwa bungeni kabla ya kuvunjwa kwa Bunge la 12 mwaka huu.
Mhe. Mchengerwa ametoa agizo hilo leo, Februari 6, 2025 katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa Soko Kuu la Majengo na vituo vya daladala jijini Dodoma kupitia mradi wa uboreshaji miundombinu ya Miji (TACTIC) awamu ya pili unaotekelezwa chini ya Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA).
Amesema Dodoma haiwezi kuwa Makao Makuu kwa matamko pekee, bali ni lazima kuwe na sheria rasmi itakayohakikisha hadhi yake inalindwa kwa vizazi vijavyo.
Amesema “Sheria hii iharakishwe kama zinavyoharakishwa sheria nyingine. Hatuwezi kusubiri tena. Tutamuomba Mheshimiwa Rais kwa hati ya dharura ili iwasilishwe bungeni kabla ya kuvunjwa kwa Bunge hili.”
About The Author
Last modified: February 8, 2025