Visit Sponsor

Written by 3:06 pm KITAIFA Views: 41

WAZIRI JAFO ATOA MAELEKEZO USAFI WA FUKWE

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt.
Selemani Jafo amewahimzia wawekezaji wanaowekeza katika fukwe
mbalimbali nchini kuhakikisha zinakuwa safi ili kutunza mazingira.
Dkt. Jafo ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kipindi cha Asubuhi
Hii kinachorushwa na kituo cha Radio cha TBC Taifa leo tarehe 19 Machi,
2024.
Amesema kuwa kumekuwepo na changamoto ya uchafu katika fukwe nyingi
nchini hususan chupa za plastiki zilizotumika ambazo si tu husababisha uchafu
wa mazingira lakini pia ni kero kwa wageni wanaozitembelea.
Kutokana na hali amezielekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa ambako fukwe
hizo zinapatikana, licha ya shughuli mbalimbali za utunzaji wa mazingira
wanazotekeleza pia zisimamie shughuli za usafi wa mazingira katika maeneo
hayo.
Waziri Dkt. Jafo ameongeza kuwa halmashauri hizo ziwe na mpango wa
kushirikiana na vijana wanaojitolea kuikota chupa zinazotupwa katika fukwe
kwa kuwapa motisha hivyo maeneo hayo kuendelea kuwa safi.
Pamoja na kutoa pongezi kwa viwanda vinavyorejeleza chupa za plastiki
amewahimiza wenye viwanda wengine kuchukua hatua hiyo ambayo itasaidia
katika kuondosha taka za chupa katika fukwe.
Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais inashirikiana bega kwa bega na wadau
mbalimbali kuwahamasisha kushiriki kikamilifu katika kuhakikisha mazingira
kwenye fukwe nchini zinakuwa safi.
Kwa upande mwingine Waziri Dkt. Jafo amewataka wenye magari kuwa na
vyombo maalumu vya kuhifadhia taka badala ya kutupa ovyo njiani ili kutunza
mazingira ya barabarani.
“Tuna kazi kubwa ya kutengeneza ustaarabu, utakuta mtu akiwa kweny basi
anakunywa maji anatupa chupa nje na inazagaa ovyo na kuchafya mazingira
hivyo tunawataka wenye magari na wenye mabasi wote kuwa ‘dustbin‘ kwa
ajili ya kuwekea taka na wenye magari simamieni zoezi hilo,“ amesisitiza Dkt.
Jafo.
Ikumbukwe kuwa awali kulikuwepo na changamoto ya chupa za plastiki
ambazo hutupwa ovyo na sasa hivi zimekuwa ni malighafi kwa viwanda kwa
ajili ya kurejelezwa.

Kutokana na hatua hiyo Serikali imekuwa ikihamasisha viwanda kufanya
urejelezaji wa chupa za plastiki ambazo huokotwa na kukusanywa katika
maeneo mbalimbali yakiwemo fukwe.

About The Author

(Visited 41 times, 1 visits today)

Last modified: February 19, 2024

Close